Baraza la diaspora wa Tanzania duniani-TDC Global linawajulisha wanachama na diaspora wa Tanzania kuwa, mkutano mkuu na uchaguzi wa viongozi wake utafanyika ana kwa ana tarehe 11 na 12 Julai 2023, Cardinal Rugambwa Social Centre uliopo Haile Selassie Road, Oysterbay Dar es Salaam. Uamuzi huo umefikiwa kupitia mikutano ya kamati kuu na bodi ya ushauri ya TDC Global yenye kumb.TDC20220627/01 na Kumb.TDC20220715/01 uliofanyika kufuatia mkutano wa Bodi ya Ushauri wenye Kumb. TDC20220703/01.

TDC Global inaomba wanachama, vyama vya diaspora, na wadau wengine kujiandaa mapema, ili kufanikisha mkutano huo muhimu kwa taasisi yetu na watanzania wote kwa ujumla. Taarifa zaidi kuhusu maandalizi ya mkutano huo zitaendelea kutolewa kwa kadri zinavyokamilika. Tunatanguliza shukrani. Mungu ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania

Jiandikishe Kuhudhuria Mkutano Mkuu

Ili kufanikisha maandalizi ya mkutano huu kwa ubora, uongozi na waandaaji wa mkutano wanahitaji kufahamu idadi wa watakao hudhuria mkutano huu. Hivyo tafadhali jaza fomu hii, ili kwa ajili ya kuwezesha maandalizi.